Showing posts with label Featured Weekly Blog. Show all posts
Showing posts with label Featured Weekly Blog. Show all posts

Kutana na Mwanablogger Augustino Chengula




Unaweza kutuambia kidogo kuhusu wewe na blog yako?
Mimi naitwa Augustino Chengula niliyehitimu shahada ya kwanza ya Tiba Mifugo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro mwaka 2007. Blog yangu inaitwa “SEKTA YA MIFUGO TANZANIA” inayobeba jina linaloendana na kile kinachowasilishwa katika blogu hiyo. Lengo kubwa la blog ni kuelimisha umma na wafugaji juu ya ufugaji na namna ya kukabiliana na magonjwa ya mifugo.

 Je, wewe kazi yako ni kublog tu au hii ni kama kazi ya muda tu au hobby?
 Kublog si kazi yangu ila ni hobby tu na lengo langu kubwa ni kuelimisha umma na hasa wafugaji juu ya mifugo na ufugaji na mambo yanayoendana na hayo. Hivyo naelimisha umma kwa kupitia fani yangu ya mifugo.

Jinsi gani unaanza kublog na kwa nini?
Kabla hata ya kuanzisha blog nilikuwa najaribu kutengeneza tovuti yangu kwa kupiatia zile za bure. Baadaye nikaona kwa kuchelewa watu wanablog na mwanzo sikujua kama ni za bure. Nilipojua kuwa ni za bure nikaanza kujifunza mwenyewe namna ya kufungua blog, nikafanikiwa. Nikawa naendelea kuiboresha taratibu kwa kuangalia blog za watu wengine zipoje. Wakati mwingine nilitumia Jamii forum kuuliza kama nataka kufanya kitu fulani kwenye blogu inakuwaje. Sikuwa na elimu ya web designing lakini nilijua kutumia vitu vya kawaida katika computer. Kupenda kujifunza vitu mwenyewe vilinisaidia. Lengo kubwa la kuanzisha ni kutaka kuwagawia elimu ya ufugaji watu wengiene kwani niliona wanahangaika kuitafuta hasa katika lugha ya kiswahili kwani mambo mengi yapo kwa lugha ya Kiingereza.

Kutana na Mwanablogger Umar Makoo


  1. Unaweza kutuambia kidogo kuhusu wewe na blog yako? Mimi naitwa Omari Abdallah Makoo na blog yangu inaitwa BUSTANI YA HABARI
  2. Je, wewe kazi yako ni kublog tu au hii ni kama kazi ya muda tu au hobby? Hapana mimi kazi yangu sio kublog tu bali ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika mwaka wa masomo utakao anza hivi karibuni pale MUSLIMUNIVERSITY OF MOROGORO
  3. Jinsi gani unaanza kublog na kwa nini? Mara ya kwanza nilipata hamasa ya kublog baada ya mhadhiri wa chuo kugusia swala la utengenezaji wa blog,faida na namna ya kutengeneza blog.Sababu iliyonisukuma kublog ni shauku ya kuhitaji kufukisha habari katika jamii mbali mbali nikiwa na chombo cha kujitemea mwenye kikiwa kama hazina ya habari.
  4. Nini changamoto unazozipata kwa kuwa na blog? Mwanzo nilikumbana na tatizo la uchache wa visitors ingawaje swala hilo halipo kwa sasa,Pia uchache wa vifaa vya kukusanyia habari pamoja na kukosa watumishi.

Featured Blogger - Sweetbert Philemon

  
Kutana na mwana blogger wetu wa week hii kutoka The Lake Zone Link

1. Unaweza kutuambia kidogo kuhusu wewe na blog yako? 
 Naitwa Sweetbert Philemon toka Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha. Nimeanza kuwa Blogger mnamo Mei 2011, ambapo ndipo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufungua blog wakati huo nikitumia Jina Best Bongo Music kama jina la Blog hiyo, lakini nilisitisha kutokana na kutokuwa na vifaa vya kutosha. Hadi mapema Mwaka huu ambao blog yangu nimeibadili kutoka This Is Habari hadi kuwa The Lake Zone Link kutokana na sehemu ambayo natokea. Nimekuwa nikijisikia furaha sana pale ninapohisi kuwa nab log na inafanya kazi. 

2. Je, wewe kazi yako ni kublog tu au hii ni kama kazi ya muda tu au hobby? 
 Kublog kwangu kumegawanyika katika aina tofauti, kwanza kwangu ni kama Hobby kutokana na kupenda sana masuala ya Information Technology, lakini pia kwangu naichukulia kama kazi yangu binafsi kutokana na kuwa nina Muda ambao nimeutenga kwa ajili ya kazi hii kama Kazi zingine nifanyazo. 

3. Jinsi gani unaanza kublog na kwa nini? 
Ili uweze kuanza kublog kwanza ni lazima uwe na akaunti ya barua pepe ya mtandao wa Gmail, baada ya hapo utajisajili vile vile kwa kutumia barua pepe katika mtandao wa Google ufahamikao kama www.blogger.com, ambapo baada ya kusajiliwa utaweza kuanzisha blog kwa ajili ya kazi hiyo. Unablog pale unapohisi unamuda wa kufanya hivyo na kuna mambo mbalimbali ambayo unahitaji kuijulisha jamii kwa namana nyingine ya kimtandao 

4. Nini changamoto unazozipata kwa kuwa na blog? 
Changamoto ninazopata kwa kuwa na blog kwanza ni Gharama za Uendeshaji kama pesa ya kuwa na vifaa mbalimbali vya kisasa zaidi kama Computer na Camera, Upatikana wa Mtandao(Network) hii ni moja ya changamoto kutokana na mazingira mengine kutokuwa na mtandao kabisa hivyo kushindwa kuifanya kazi, Upatikanaji wa Habari unakuwa mgumu kwani inabidi muda mwingine kutumia habari zilizokusanywa na wanablog wengine, Kufahamu mahitajio ya mashabiki, wakati mwingine inakuwa ngumu kufahamu ni nini wadau wako wanahitaji kutokana na kutoacha maoni yoyote katika sehemu ya maoni, hivyo kufanya kazi kwa kubuni, Mwisho ni muda inafikia kipindi inabidi kutumia muda wa shughuli nyingine katika kublog kutokana na Habari inahitaji kuandikwa muda gani. 

5. Ni miaka mingapi sasa umekua ukiblog? 
Ni Mwaka mmoja na Nusu tangu nimekuwa nikiblog 

6. Unafanya nini wakati ukiwa hushughulikii hii blog yako? 
Wakati si shughulikii blog hii nafanya majukumu mengine ya Kishule na Nyumbani pia ili kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa, bila kupoteza kimoja wapo. 

7. Ni mara ngapi unafikiri juu ya blog yako wakati uko mbali na kompyuta?
Inajirudia kwa mara nyingi kufikiria kuhusu blog yangu pale ninapokuwa niko mbali na Kompyunta hasa kuhusu Mwonekano wake, Habari zilizopo na Wadau wangu wa blog. 

8. Ni nani wasomaji wa blog yako? 
Asilimia kubwa ya wasomaji wangu ni Vijana kutokana na Habari za kiburudani ambazo zinakuwepo. 

9. Je ni mitandao gani mingine ambayo unatumi ili iweze kukusaidia kuitangaza blog yako ili iwafikie wasomaji walengwa wa blog yako? 
Mfani Twitter au Facebook Mitando migine ambayo natumia kuitangaza blog yangu ni pamoja na Google Plus, Alexa, Networkedblog pamoja na facebook na Twitter 

10. Nini hasa ni changamoto kubwa wakati unatengeneza post ya kuweka kwenye blog yako na kwanini? 
Changamoto wakati wa kutengeneza post ni pale unapokuwa unatumia post kutoka kwa wanablog wengine, kwani itakuchukua mrefu sana mpaka kuikamilisha post hiyo, Mfano kupata picha zinazoendana na post hiyo, kuweka sauti za muziki ambapo itabidi uingie katika mitandao mingine kutafuta vitu kama hivyo. 

11. Unafanya nini iwapo kuna wakati huna la kuandika kwenye blog yako? 
Wakati sina la kuandika katika blog yangu, huwa nafanya marejeo katika blog yangu kuangalia makosa ambayo yamejitokeza na pia kuangalia vitu vya kuongeza na kupunguza katika designing(Mwonekano) wa blog yangu ili iendelee kufana. 

12. Je ni nini mkakati wako na blog yako kwa ujumla? 
Mkakati mkubwa uliopo katika blog yangu, kwa ni kuifanya Website ili uwe ni mtandao mkubwa ambao utakuwa na kazi ya Kuhabarisha jamii mambo mbalimbali,Hadi kufikia hatua ya kuweza kaujili vijana wengine kushirikiana katika kazi hii, kama ilivyo mitandao ya Habari mingine mikubwa Duniani mfano ABC. 

13. Je ni bora kupata ukweli au uchunguzi wa jambo unalotaka kuliandika kwenye blog yako wewe mwenyewe au kupitia mtu mwingine? 
Ni bora kupata ukweli au uchunguzi wa jambo mwenyewe, hii itasaidia katika kuwa na uhakika na kile ambacho unakifanya, Lakini pale inapohitajika mtu mwingine kuwa na ukweli huo unaweza kuutumia labda kutoka na namna ya kukamilisha uchunguzi huo. 

14. Ni jambo gani bora blogger anaweza kutoa kwa wasomaji wake? 
Jambo bora ambalo blogger anaweza kulitoa kwa kwa wasomaji wake, ni jambo ambalo linawasaidia wasomaji na kuwapa uhakika wa jambo fulani ambalo walikuwa hawalijui au wana mashaka nalo, hivyo kuwafanya wapate uhakika huo, na kuweza kuwasaidia. 

15. Ni jinsi gani (mtu) anaweza kuelezea style ya yako unavyo blog? 
Mtu anaweza kuelezea style yangu ya kublog kwa namna tofauti tofauti kama, Uhabarishaji wa jamii, Kuburudisha jamii lakini pia anaweza sema ni kuonyesha uwezo wangu katika masuala ya mitanda 

16. Ni nini imekuwa mkakati wako kwa ajili ya kujenga kujulikana kwa mwenyewe na blog yako? 
Mkakati wa kwanza ni mimi mwenyewe kujitambulisha ndani ya blog ili watu kunifahamu pale wanapoitembelea, lakini pia mkakati wa pili ulikuwa nia Ukurasa wangu facebook ambao unanitambulisha kama mmiliki wa blog hiyo, pia twitter na mkakati mkubwa ni kupitia Tanzania blog Directory List ambapo blog yangu nimeitambulisha huko, Lakini pia ni katika mtandao wa Google na njia ya Jamaa zangu walio katika Media. 

17. Kila mtu ana post anayoipenda au anayoichukia. Je wew ni post ipi unaipenda sana na kwanini? Na ni post ipi unaichukia sana na kwanini? 
Napenda sana post ambayo imejaa uhalisia wa picha na video pamoja na maneno ambayo itatoa uhakika zaidi. Nachukia post iliyojaa maelezo pekee kwani msomaji hatapa kuhakiki kwa kutumia vithibitsho halisia. 

18. Je ni bloggers wapi ambao wewe unawaangalia na kufuata nyayo zao? Na kwanini?  
Bloggers ambao mie nawafuata ni pamoja na Dj Choka kutokana na namna anavyotoa mchango wake katika sanaa ya Muziki hapa nchini, lakini pia Millard Ayo kutokana na aina yake kuwahabarisha wasomaji kwa namna tofauti katika mtandao wake na kuwa update kwa kiasi kikubwa na Mx Carter wa Gonga Mix kutokana na namna ya mwonekano wa mtandao wake, hivyo kupitia kwao najifunza mambo mengi 

19. Hebu tuambie ni watu gani umewahi kukutana nao wakati ukisughulikia post za kuweka kwenye blog yako?
Nimekutana na Jamaa yangu Mtaki R Myenjwa pamoja na Norles Wales kipindi hicho nilikuwa nafuatilia post inayohusu ufunguzi wa Jiji la Arusha. 

20. Je unafikiria kuwa unadaiwa na mtu akiyeacha comment/s kwenye blog yako?
Ndiyo nitakuwa na daiwa kuijibu comment hiyo ili kuonesha ushirikiano wangu na wasomaji wangu 

21. Je kunadhamani kujibu comment iliyoachwa kwenye blog yako wakati ukijua kuwa huyo aliyeiandika labda hatarudi kusoma jibu lake tena? 
Thamani ipo kwani kuwepo kwa comment hiyo na kuijibu kutasaidia na wasomaji wengine wakuachie pale comment zao ambazo zitakusaidia katika maboresho mbalimbali ya blog yako na pia kutambua ni jinsi gani watu wanaitembelea. 

22. Je, umewahi kufikiria kuacha kupost comment ambayo iko negative kwako na ukijua hamna mtu atakayejua? 
Hapana sijawhi fikiria hilo kwani itafanya wasomaji wengine waone naruhusu upuuzi katika blog yangu. 

23. Je unazitreat tofauti au unafikiri watu wanaoacha comment kwenye blog yako na kuacha majina yao yaonekane wazi wanastaili comments zao kujibiwa au hata kuacknowledge kuwa umeona maoni yao? 
Kila kitu nisawa kwa yule aliyeacha au ambaye hajaacha jina , ikiwa tu comment zao zina maelezo yenye kuhitaji majibu. 

24. Je, unafikiria ni makosa kucomment kwenye blog yako kwa kutumia jina lingine? 
Sio makosa kwani ni kama njia yakuonyesha msomaji wako mpya nini atafanya katika eneo kama hilo katika blog. 

25. Je unazichukulia comments zote sawa unazotumiwa kwenye blog yako bila kujali maoni uliachwa?
Hapana Comment zote haziwezi kufanan kila moja itakuwa na ujumbe wake hivyo inabidi kujali zaidi maoni yaliyoachwa kufahamu utafanya nini. 

26. Je, unaamini comments kwenye blog yako zilizoandikwa kwa urefu sana zinahitaji kuzawadiwa zaidi kuliko zile zilizoandikwa kwa ufupi tu? 
Sio kweli urefu wa comment sio kwamba ndio imeendikwa kitu kikubwa ndani yake,bali hata comment fupi inaweza kuwa na ujumbe mzito kwako na wa kuufanyia kazi zaidi. 

27. Je wewe ni mtu ambaye uko rahisi kukata tamaa? 
Kwangu sio rahisi kukata tamaa, kutokana na mihangaiko ambayo nimeipata katika kublog, nitaendlea kuwepo. 

28. Je unaedit picha zako ili ziwavutie sana wasomaji?
 Hapana napenda zaidi picha iliyo na uhalisia kwa msomaji, lakini pale inapohitajika kufanya hivyo huwa na edit. 

29. Je unaepuka kuweka post ambazo ziko very controversy kwasababu ya kuogopa watu hawatakubaliana na wewe au huna hizo post? 
Naepuka kuafanya hivyo lakini inapofikia hatua ya kuzingatia maslahi ya jamii, inabidi kufanya hivyo. 

30. Je unajisikia vizuri zaidi ukiweka post kwenye blog yako na ukapata maoni ya watu zaidi ya 20 au ukipata maoni ya mtu mmoja mashuhuri tu. 
Najisikia faraja sana pale ninapopata comment hata moja tu lakini yenye maoni ya kunijenga zaidi katika blog yangu na siyo kujali wingi na umashuhuri wa mtu 

31. Je unasema blog yako kuwa inamafanikio iwapo unapata watu wengi wa kusoma au unapata watu wengi wakuacha comment kwenye blog yako? 
Blog itakuwa na mafanikio zaidi pale inapopata wasomaji wengi zaidi kwani itatangazika katika watu wengi na kufikia watu wengi zaidi, zaidi ya kuwa na comment za wasomaji wachache ambao hawataitangaza blog yako zaidi 

32. Je blog yako unatumia jina lako kamili au unablog kwa kutumia kivuli kingine na watu wanasoma na kuenjoy blog yako lakini hawajui wewe ni nani? 
Natumia jina la Kanda ya ziwa The Lake Zone Link, kutokana na sehemu ambayo natokea mkoa wa Mwanza na watu wanaenjoy kuona nawakirisha kanda hiyo. Wanatambua mimi ni nani kutokana na utambulisho ulio ndani ya blog. 


33. Ni nini baadhi ya malengo yako ya mwaka huu kwa ajili ya blogu yako au unaonaje mwenyeew kwa kipindi cha mwaka mmoja ua mitano toka sasa hivi blog ya itakuaje? 
Nina Malengo ya kufanya jitihada za kupata vifaa vipya vya kuendeshea blog hii kama Laptop/Kompyunta, Camera, Moderm na vitu vingine ambavyo vitahitajika,ili kuanzia mwaka huu na kuendelea blog hii iwe ni moja ya mitandao ya kijamii mikubwa nchini kwa watumiaji wa mitandao. 

34. Je upi ujumbe wako kwa wale watu wanaotaka kuanza kublog? 
Ujumbe ni kuwa kwanza wajiandae kikamilifu hasa kuwa na vifaa vya kuendeshea blog na wala sio mahudhurio ya internet cafe, itawagharimu pesa nyingi, ni heri kuwa na vifaa vyako mwenyewe. Na pia hizo blog zao wazisajili ili ziweze kutambulika Nchini. 

35. Je kwa maoni yako ni lengo gani kubwa kwa mwanablogger? 
Lengo kubwa kwa wanablogger tutumie nafasi hii kujitoa kwa sehemu ambazo tunaona zimefumbwa katika jamii zetu hivyo kuibua sauti zao, na kufikisha ujumbe wao, hasa katika kutetea haki za jamii nzima

36. Watu wengi wanafikiria kublog kwa ajili ya kupata hela. Je ni nini baadhi ya vidokezo kwa watu wanaofikiria kufanya hivyo? Je, ni ukweli upi wa baadhi ya matarajio yanayohusina na nini kinaweza kufanywa na nini hakiwezi kufanywa wakati wa kublog? 
Kublog si kwa ajili ya kupata pesa pekee kama watu wengine wanavyodhania zaidi, bali kublog ni namna ya kuisaidia jamii katika sekta mbalimbali kupata sauti itakayowafikia walengwa. Wakati wa kublog huwezi fanya mambo ambayo hayana interest na jamii.

Asante sana na tunakutakia mafanikio mema katika masomo yako na pia katika blog yako. 

Featured Blog - Suleyman Omary

Mimi naitwa Suleyman Omary lakini ni maarufu kwa jina kbornz au Sme ni mkazi wa Dar es Salaam, ni miliki wa blog ya Kbornz Blog

Nimekua blogger kwa muda wa mwaka 1 sasa ila niliifungua hii blog mwaka 2007, nikaachana nayo sababu nilikuwa sina muda na access ya internet kwa ajili ya kuupdate habari kila siku. Kiukweli nilivutiwa kuanza blogging baada ya kumuona Mjengwa kipinde kile anakuja ofisini kwetu pale kinondoni Cavalli internet so nikaamua na mimi nijaribu. Nilivyojaribu sikukaa muda nikaachana nayo, sasa nimerudi kwa nguvu mpya kabisa.
Ili kufanya blog yangu ijulikane zaidi, natumia mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter na mtandao wa Google plus. Mikakati niliyonayo kwa ajili ya blog ni kupata wasomaji wengi zaidi na blog yangu kuwa miongoni mwa blog maarufu hapa Tanzania na pia nje ya Tanzania.

Hata kama sina picha za matukio husika hua natafuta picha za wahusika kupitia mitandao mingine ili kufanya post ziwe na mvuto zaidi. Ninachoamini ni kwamba, picha zinahabarisha zaidi ya maneno, na zinaleta mvuto kwa msomaji pia kuendelea kusoma na kumfanya arudi tena kwa siku zingine.


Tanzanian Blog Awards inakutakia mfanikio mema katika blog yako. Tafadhali tembelea blog yake kwa support na maoni. www.kbornz.blogspot.com

Mwanablogger wa week hii ni Ngwesa Paulo

Naitwa Ngwesa Paulo ni mhitimu wa chuo kikuu nina shahada ya utalii. Naishi Morogoro niliamua kuanzisha blog ambayo itakuwa inatoa habari mbalimbali kuhusiana na utalii Tanzania ili kuhamasisha utalii wa ndani na nje pia utupe faida mana tunavivutio vingi sana.

Kublog kwangu ni kama kazi wala sio kama hobby, kublog nilianza kama miezi sita iliyopita nilianza na blog inayokwenda kwa jina la Hapa hapa Tourism nikaona haileti maana niliyokusudia ndio nikanzisha hii ya NGWESA.

Kitu kilichonisukuma nianze kublog ni pale nilipoona hapa Tanzania tuna vivutio vingi sana lakini bado havijulikani waliopewa hiyo zamana hawaifanyi nikaona naweza fanya kazi hii kirahisi kwa kutumia blog.

Changamoto ninazozipata katika kazi hii ni ukosefu wa vitendea kazi vya uhakika kama kamera
zenye uwezo, ukosefu wa wazamini wa kudumu katika kazi hii kwa ujumla.

Wakati sighuliki na kazi za hii blog nafanya kazi zingine za kimaisha na mara nyingi nikiwa mbali na kompyuta huwa nafikilia sana blog yangu.

Wasomaji wa blog yangu ni watu wote tu Duniani kwa ujumla mana ni ya mambo ya kitalii hayana mkubwa wala mdogo.

Ili habari za blog hii ziwafikie watu wengi zaidi huwa natumia mitandao ya jamii kama facebook pamoja na twitter pia huwa nawaomba watu wenye blog zinazojulikana kuwatangazia wasomaji wao kama kuna blog nyingine ya mambo ya kitalii.

Changamoto kubwa wakati wa kutengeneza post ninayopata nazani network na pale ninapojiuliza je hii post itafaa , inapotokea sina la kuandika kwenye blog huwa naacha tu kwa siku hiyo ili niweze kutuliza akili nisije haribu mana kazi hii inatakiwa umakini mkubwa sio kucoppy na kupaste.

Mkakati wangu ni kuutangaza utalii wa Tanzania ujulikane zaidi mana bado upo chini pia blog yangu ijulikane na watu wengi kimataifa.

Katika kuweka habari ni bora kupata ukweli au uchunguzi wa jambo ambalo blogger anataka kuweka kwenye blog yake kupitia watu wengine au yeye mwenyewe. pia jambo mhimu ambalo blogger anaweza wapatia wasomaji wake ni habari zenye uhakika zaidi.

Style yangu ninayotumia kublog ni habari zinazoambatana na picha siunajua katika habari kama hizi za kitalii picha ni mhimu sana na maelezo yake kidogo.

Ili kujenga kujulikana mimi na blog yangu nimekuwa nikipost vitu vizuri ambavyo vinaweza kuwavutia watu wengi zaidi ili kuwafanya wapende kutembelea blog yangu kila mara pia huwa nawaomba watu wenye blog zinazojulikana zaidi kuwajulisha wasomaji wao kama kuna blog hii ya mambo ya kitalii pia.

Katika kupost ni kweli kila mtu anapest yake anayoipenda na nayoichukia kwa upande wangu post zangu zote nazipenda mana ni utalii tu kwa sana sijui kama zinachukiza.

Blogger ninaowangalia na kuwafata nyayo zao ni Issa Michuzi, Dj Choka , Bukopasport hawa nawapenda kwasababu waipenda kazi yao kublog kwao ni kazi pia ukiwa na shida kuhusiana na blog sio wagumu kukusaidia.

Nimekuwa nakutana na watu wa aina mbalimbali ambao hunikatisha moyo na wengine hunisupport wakati nasghulikia post zangu lakini sio mabya ndivyo ilivyo.

Mtu akiacha comment inayodai marekebisho ushauri nazani anahitaji kuona kitu alichokuambia ukikifanyia kazi na comment zingine huwa hazihitaji majibu mana huwa ni za kukupongeza tu.pia kuna dhamani kubwa kujibu comment iliyoachwa na msomaji hata kama hatarudi kusoma tena wengine ataiona kama ilijibiwa. Wasomaji wanaoacha comment kwa majina yao nazani kuwaacknowledge ni vizuri zaidi.

Pia sio makosa msomaji kucomment kwa kutumia jina linguine mana kinachohitajika comment na si jina la mhusika,

Mimi sio mtu wa kuakata tama kirahisi mana kukata tama nafanisha na kosa kubwa kama padre kumbaka muumini wake ni hatari sana, watu wanaokata tama wanahatari kubwa sana katika maisha yao.

Picha zangu ninazoweka katika post ni picha za uhalisia mana huu ni utalii uhitaji edit wala nini uhalisia ndo mpango.

Katika hii blog yangu nazani sina post post ambazo ziko very controversy kwa hiyo ni amani tu mimi na wasomaji wangu kitalii tu zaidi.

Huwa najisikia faraja sana ninapo weka post na kupata maoni ya watu wengi mana inaonesha kazi yangu imekubalika kwa watu wengi zaidi. Swala la wat mashuhuri wanaruhusiwa kutoa maoni pia kama watu wengine tu.

Katika kupost habari na kitu chochote kwenye blog yangu natumia jina langu harisi mana hii ni kazi kama kazi zingine uhuni uhini hautakiwi katika ofisi yoyote naheshimu ofisi yangu.

Baadhi ya malengo ya blog yangu kwa mwaka huu ni kuifanya ijulikane zaidi na watu wengi imataifa.baada ya mda natumaini itakuwa blog bora kwa mambo ya kitalii hapa Tanzania.

Ushauri wangu kwa wale watu wanaotaka kuanza kublog ni kutafuta wazo jipya katika kufanya kazi hii sio kucopy na kupaste sio vizuri ze comedy wanaweza waona na kuwatania.

Mi nazani lengo kubwa la wanablogger wengi ni kupata wasomaji wengi zaidi na kazi zao kujulikana zaidi ili iweze kuwa kazi ya kuwaingizia kipato.

Mwana blogger wa week hii ni Nixl Carter



Mimi naitwa Nickson Lema lakini ni maarufu kwa jina Nick au Nixl Carter ni mkazi wa Moshi.

Nimekua blogger kwa muda wa mwaka 1 na nusu .Kiukweli Nilivutiwa kuanza blogging baada ya kuwa napata habari mbalimbali na kuona zinafaa kuwafikia watu wengine so nikawa pia na muda wa kufanya blogging, pia ubunifu wangu uliniruhusu kuweza kuanza na kupata idea nzuri. Kwa Kuanza nilianza na blog ya Jokes na Funny stories (SUPAJOKES) www.supajokes.blogspot.com lakini nikawa pia interested na issue za entertainment nikaona ni vyema niwe na blog kuhusu burudani,music,habari na pia chatting, ndipo mwaka wezi wa tisa mwishoni nikaanzisha blog ya (BONGO SWAGGZ) www.bongoswaggz.blogspot.com

Kutana Na Mwanablogger Wa Week



Week hii mwanablogger wetu ni Tryphone Chasama anayeishi Dodoma. Tryphone Chasama ni mmiliki wa blog ya BongoNewz Blog. Blog yake inahusu habari, burudani, habari za jamii na siasa kwa ujumla.

Ifuatayo ni historia fupi ya Tryphone na pitia blog yake BongoNewz Blog kusupport na kufahamu mengi kuhusu blogger huyu:-

“Elimu yangu ni Shahada ya sayansi (BSc Education) na kwa sasa ninaendelea na masomo ya shahada ya pili katika chuo kikuu cha UDOM. BLOG yangu inaitwa BONGONEWZ BLOG, niliianzisha mwaka jana lakini sikupata muda mwingi zaidi wa kuifanyia kazi mpaka mwezi Julai mwaka huu ambao ndio nilipata muda zaidi wa kuishughulikia na mpaka sasa nina muda mwingi wa kuishughulikia. Blog yangu kama nilivyosema inatumia kivuli lakini jina langu lipo kwenye blog sehemu iliyoandikwa (about me) na hapo nimejielezea vizuri mimi ni nani.

Nimekua nikiblog kwa muda wa mwaka sasa na kitu kilichonifanya nianzishe blog ni hali tu ya kuipenda hii kazi kwani ni kazi ambayo nilipanga nije kuifanya. Kwa sasa sina kazi nyingine zaidi ya kublog na ninaifanya hii pia kwa ubunifu wa hali ya juu kwani zaidi ya kuwa ni kazi yangu pia ni hobby vilevile.


Changamoto niliyonayo katika kublog ni kupata habari, pia vitendea kazi
kama kamera ni changamoto kwangu. Wasomaji wa blog yangu ni watu wa rika zote kwani blog yangu ina habari zinazomhusu kila mtu.

Ili kufanya blog yangu ijulikane zaidi, natumia mitandao ya kijamii
kama Facebook, twitter na mtandao wa Google plus. Mikakati niliyonayo kwa ajili ya blog ni kupata wasomaji wengi zaidi na blog yangu kuwa miongoni mwa blog maarufu hapa Tanzania na pia nje ya Tanzania.

Style ninayotumia kublog ni ile inayoambatana na picha za matukio husika au hata
kama sina picha za matukio husika hua natafuta picha za wahusika kupitia mitandao mingine ili kufanya post ziwe na mvuto zaidi. Ninachoamini ni kwamba, picha zinahabarisha zaidi ya maneno, na zinaleta mvuto kwa msomaji pia kuendelea kusoma na kumfanya arudi tena kwa siku zingine.

Bloggers ambao wamekua
kama dira kwangu na ambao natamani nipite katika njia walizopita ni Issa Michuzi, Magid Mjengwa, Haki Ngowi na John Bukuku. Nawapenda sana hawa Bloggers kwa sababu ya kazi wanazozifanya. Kublog imekua ni kazi kwao na wanaifanya kazi hii kwa umakini mkubwa.

Mtu akiacha comments kwenye blog sio lazima nimjibu ila itategemea na aina ya comment aliyoacha kwani kuna comments zingine zinahitaji majibu, na baadhi ya comments hua ni maoni tu ya mhusika kuhusu post iliyopo kwenye blog…Lakini comments zinazohitaji majibu hua nakuwa makini sana kumjibu kwa wakati kwani nahisi ni kama deni kwangu na hua najisikia vizuri sana kumjibu. Kujibu comments za wasomaji ni kitu cha thamani
sana haijalishi kama atarudi kusoma au la, kitendo tu cha kujibu comments kitamfanya msomaji arudi tena na tena na awe na uhuru wa kucomment juu ya kitu chochote kile anachofikiria.

Kukata tamaa katika maisha yangu ni kitu ambacho naona ni kosa kubwa
sana, siwi mwepesi kukata tamaa hata kama kazi ninayofanya inakua na changamoto nyingi sana. Malengo yangu kwa mwaka huu ni kuwa na wasomaji wengi zaidi, na kwa kipindi cha mwaka mwingine ujao blog hii itakuwa miongoni mwa blog zenye wasomaji wengi zaidi hapa Tanzania na hata nje ya nchi.

Ujumbe wangu kwa watu wanaotaka kublog ni kutosita kuanza kazi hii kwani ni kazi
kama ilivyo kazi nyingine. Na wasikate tama pale wanapokutana na changamoto mbalimbali.

Lengo kubwa kwa mwanablogger yeyote ni kuwa na idadi kubwa ya wasomaji na blog yake kujulikana zaidi….na zaidi ya hapo ni kuifanya kazi ya kublog kuwa kazi inayomwingizia kipato.”

Tanzania blog Awards inakutakia mafanikio mema katika masomo yako na blog yako kwa ujumla.

Meet Nicko J. Mhapa - Our Weekly Featured Blogger

Happy Friday! Welcome to our weekly blogger interviews on the Tanzanian Blog Awards. Today our special thanks to Nicko Mhapa for taking the time to sit down and answer these questions.

Kutana Na Mwana blogger wa week hii Ally Msangi

Hello everyone  na karibuni katika mahojiano yetu ya kila week. Week hii tumepata bahati ya kufanya mahojiano yetu na mwanablogger anaye miliki blog ya Jobs Tanzania. 

Karibu sana hapa na tunafurahi sana kufanya mahojiano yetu hapa na wewe. Hebu tuanze mahojiano yetu kwa kuteleza kidogo kuhusu wewe binafsi na blog yako?

Kwa jina naitwa ALLY MSANGI, Ni mwanafunzi wa mwaka wa 3 katika chuo kikuu cha SAUT (St. Augustine University of Tanzania). Nachukua shahada ya kwanza katika masomo ya Biashara (BBA). Blog yangu inajulikana kwa jina la JOBS TANZANIA BLOG ikiwa ni mahususi kwa ajili ya kutangaza nafasi mbali mbali za kazi. Na wasomaji kuweza kuzisoma nakuomba kazi hizo. Blog hii inarahisisha adha ya kuhangaika kununua magazeti kila siku na kuangalia nafasi za kazi, hivyo kwa anae taka kusoma nafasi za kazi zinazo tangazwa anapitia katika blog yangu nakuangalia ni kazi ipi ina mfaa na kuweza kutuma maombi katika anuani husika kwa urahisi zaidi

Mwanablogger wa week hii - Emu Three kutoka Diary Yangu Blog

Karibuni katika mahojiano yetu ya kila week. Week hii nimepata bahati kufanya mahojiano na Emu Three ktoka blog ya Diary Yangu. Kama wewe ni mpenzi wa riwaya natumaini mara ukiifahamu hii blog kila siku utajikuta utarudi kusoma hadithi moto moto anazoziandika Emu Three.

Karibu hapa na tunafurahi kuweza kufanya mahojiano na wewe. Unaweza kutueleza kidogo kuhusu wewe na blog yako?
Mimi naitwa emu-three, na nimetumia emu-three kama ufupisho wa majina yangu matatu yaani jina la kwangu la baba na la ukoo yote yakianzia na herufi M. Na wakati naanzisha hii blog, nilikuwa nawaza niweje jina gani , na mara likanjia jina hilo la miram3. Mira ikiwa ni jina langu halisi kwa kifupi na m3, ikiwa M.M.M.

Meet Faith Hilary - Our Weekly Featured Blogger

Karibuni sana katika mahojiano yetu ya kila week. Leo tumepata bahati ya kufanya mahojiano  yetu na mwanablogger Faith Hilary wa Candy1's Little World Blog.  

Faith asante sana kwa kukubali kufanya mahojiano haya na sisi na karibu sana.  Je unaweza kutuambia kidogo kuhusu wewe na blog yako?

Naitwa Faith Hilary, jina la utani najulikana kama candy1 na kwa jina hilo ndio nilitunga jina la blog yangu candy1world. Candy1world blog inahusika na mambo makuu manne ambayo ni habari, burudani, fashion na fun ambayo sana ni vitu vya kuchekesha wanavyofanya watu wengine; pia naandika articles tofauti au huongea na kuuliza maswali kwenye video.

Featured Weekly Blogger - Josephat Lukaza

Karibuni katika mahojiano yetu ya kila week. Leo hii tumepata bahati ya kufanya mahojiano yetu na mwanablogger JOSEPHAT LUKAZA ambaye ana miliki blogu ya LUKAZA BLOG. Karibu sana hapa na tunafurahi kufanya mahojiano nawe

Unaweza kutuambia kidogo kuhusu wewe na blog yako?
Kwanza kabisa napenda kuchukua nafasi kujitambulisha tena naitwa Josephat Lukaza. Na mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa pili sasa wa Chuo Kikuu Cha Dodoma. Nafanya shahada ya kwanza ya elimu ya jamii (Sociology). Nimeanza kublog baada ya kuhitimu masomo yangu ya kidato cha sita mnamo mwezi wa 3 mwaka 2009. Kutokana na kutokojua labda umuhimu wa blog sikuweza kuona umuhimu wakuwa na blog hapo mwanzoni lakini baada ya kuanza masomo yangu katika chuo kikuu ndio nilipoanza kufikiria kitu ambacho kinaweza kunitofautisha mimi na wengine ndipo hapo nilipoamua sasa kuanzisha blog nyingine sasa ambayo ndio hii ya LUKAZA ya link http://josephatlukaza.blogspot.com lakini haya yote niliweza kuyafanya baada ya kuweka umakini na kuchukulia hii kama sehemu ya kazi yangu na kupenda kujifunza juu ya blog na maswala mazima ya teknolojia na ndipo nikaanzisha rasmi blogu hii. Blog hii niliitengeneza mwenyewe mnamo tarehe 18 October 2010 wakati nipo likizo ndefu ya kumaliza mwaka wa kwanza wa masomo na mpaka sasa ina miezi 9 na siku kadhaa ikienda mwezi wa 10.

Featured Weekly Blogger - Abdallah Hamdun Ibrahim Sulayman

Karibuni katika mahojiano yeu ya kila week. Leo hii tumepata bahati ya kufanya mahojiano yetu na mwanablogger Abdallah Hamdun Ibrahim Sulayman ambaye ana miliki blog tatu....Ya kwanza ni Tanzania Football Event, Mashabiki wa Azam FC na Aboodmsuni Home. Karibu sana hapa na tunafurahi kufanya mahojiano nawe. Hebu tueleze kidogo kuhusu wewe na blogs zako?

Mwana Blogger Wa Week Hii Ni Sarah Crystal

Week hii tumepata bahati ya kufanya mahojiano yetu ya kila week na mwanablogger Sarah Cristal wa Agalia Bongo. Sarah ana blog yake inayokuja juu na tulifurahi sana kufanya mahojiano haya na sisi.Sarah karibu sana na tunashukuru sana kwa kukubali kufanya mahojiano na sisi. Unaweza kutuambia kidogo kuhusu wewe na blog yako?

Mwana blogger wa Week Hii - Ernest Makulilo

Week hii tumebahatika kufanya mahojiano yetu hapa na mwanablogger Ernest Makulilo. Ernest Makulilo ni mwanablogger anayemiliki blog ya  Makulilo Jr inayojishulisha na mambo ya scholarships. Kama hujawahi kuipitia na kuisoma hii blog na wewe ni mmoja wa watu wanaotafuta , wanaofikiria kupata elimu ya juu au wewe ni mzazi unayetafuta jinsi ya kupata scholarship kwa mwanao basi jitahidi ukipata muda upitie hii blog yake. Blog yake pamoja na kupublish scholarships mbalimbali bali pia ina maelezo mengi sana ya maana ya kutahadharisha watu wasije kutapeliwa wakiwa wanatafuta hizi scholarships. Ernest tunashukuru sana kwa kukubali kufanya mahojiano haya na sisi.Je unaweza kutwambia kidogo kuhusu wewe na blog yako?

Mwana Blogger Wa Week Hii - Nova Kambota

Karibuni katika mahojiano yetu ya kila week. Week hii tunafurahi kuwaletea mahojiano yetu na blogger kijana machachari sana ambaye blog yake kwa ujumla inazungumzia mambo ya siasa  jina lake ni Novatus Kambota wa blog ya  Nova TZ Dream.
 
Unaweza kumpata kwa Facebook hapa au tafuta Novatus Kambota, mfuate twitter hapa au kwa kutumia ID Name yake NovaKambota na You tube anapaikana kwa jina la  Mr Kambota. 

Meet Teen Blogger Aidan Leonce

Hey guys!!! Here is a special treat for our weekly interviews. I hope all of you are having a great weekend while are busy voting for your favorite blogs.  In recent times, blogging has become more and more accessible, therefore making it much easier for anyone to start one. It is so easy to see teenagers have found their way blogging in many countries but not in Tanzania. We are still a little behind on this.

I was a little puzzled, a little disappointed and disbelieved when we didn’t receive any nomination under the Tots category that was meant for anyone who was between the ages of 12-18 yrs old. Today I’m so thrilled to have Aidan on our weekly interviews and I am so proud to announce that he is a truly our first known product of The Tanzanian Blog Awards. Serious, I am not bragging but I am just telling the really story about Aidan. I received his email two days ago as he was so excited to found out his blog was one of the blogs nominated for the best design blog. 

Weekly Blogger Interview: Twaha Hamisi

Happy Friday! Welcome to our weekly blogger interviews on the Tanzanian Blog Awards. Today our special thanks to a very talented and promising young artist Twaha Hamisi of  Twanzania Blog for taking the time to sit down and answer these questions and make it happens. Welcome Twaha we are glad to have you here. Lets begin by telling us a little about you and your blog?
My blog is basically about inspiration, designs and lifestyle. In those subjects, you might find some graphical works, inspiring articles, entertainment news and cartoons, all done by me.


Are you a full time blogger? How did you get into blogging and why?
I am not a full time blogger. I just do it part time and I entered into blogging when I found out I have so many things to take out of my mind and heart. Provided that the people I wanted to share with my feelings and thoughts were most of the time on social medias, so blogging was the right channel for me.

Mahojiano na mwana blogger wa wiki - Amani Masue

Wiki hii tumepata bahati ya kufanya mahojiano yetu ya kila wiki na mwana blogger kutoka blog ya Amani Masue. Asante sana kwa kufanya mahojiano haya na sisi. Hebu tueleze kuhusu wewe na blog yako. Kwa jina natambulika kama Amani Masue pia ndo jina la blog yangu ni blog yenye aina nyingi za habari zikiwemo za kitaifa na kimataifa katika nyanja mbalimbali michezo,siasa,burudani n.k.
Je, wewe kazi yako ni kublog tu au hii ni kama kazi ya muda tu au hobby?
Kazi yangu sio kublog hii ni hobby tuu kuwa blog na naipenda sana kwani ninakua face to face na kila aina ya habari kila siku.
Nini changamoto unazozipata kwa kuwa na blog?
Nimepata changamoto ya kutafuta habari za kila siku,kujua leo kuna nini na kesho kutakua na nini pia japo muda wa kuhabarisha uko limited basi muda unaopatikana unatumika ipasavyo katika kupost habari.

Mwana blogger wa wiki hii ni Evarist Chahali wa Kulikoni Ughaibuni

Leo tumepata bahati ya kufanya mahojiano na Evarist Chahali wa Kulikoni Ughaibuni na kwenye Twitter anapatikana kwa jina la Chahali. Toka nimefahamu hii blog mimi personal nimekua nikiifuatilia na nilipokea email kutoka kwa wasomaji wake wapenzi wanaoifuatilia na kupendekeza kama tutaweza kufanya mahojiano naye lakini hata mimi nilikua nina mpango wa kumwandikia ili tufanye mahojiano naye. Nilikua natamani sana mahojiano haya ili watu ambao hawajawahi kuiona hii blog yake wapate kuifahamu. Ni blog yenye mambo mengi sana na anajadili mambo yake vizuri sana, kwa upana na kama inavyotakiwa (Tell it like it is). Kama hujawahi kuisoma blog yake basi usiache kuingia na kuisoma. Asante sana Evarist kwa kukubali kufanya mahjiano na sisi unaweza kutuambia kidogo kuhusu blog yako?