Jinsi ya kupata wasomaji wa kudumu
AIDS And Black Community
Blog nyingi feed updates zao hazifanyi kazi ni kwa nini?
Kwa wale wanaohitaji picha za bure hizi ni baadhi ya sites muhimu kuzifahamu
How To Thank A Blogger.
Je Wafahamu Hili?
Missing Pieces or Missing Links?

Hizi ni orodha ya mada ambazo mimi kwa upande wangu naona bado hazijazungumziwa kwa wingi sana au hazipo kabisa katika jamii yetu. Tafadhali kumbuka kuwa hii sio repoti ya kisayansi na ninafahamu kuwa kuna blog nyingi tu za kitanzania bado hatujafanikiwa kuzipata ili tuziorodheshe kwenye directory list yetu. Hapa kwenye list yetu kwa kuangalia kwa haraka haraka karibu tumeshaziorodhesha kama 50% tu ya blogs zinazoandikwa na watanzania mpaka sasa hivi.
Mimi kama mwandishi wa hili shindano nimeshapitia hizi blog zote kwa zaidi ya mara moja hivyo ninaweza kusema kwa uhakika kuwa mpaka sasa hivi hizi mada zimepungua au hazijazungumziwa na watu wengi. Hizi mada najua kuna wasomaji wengi sana tu wangependelea kusoma mabo kama haya. Kama mtu akiamua kufungua blog na kuzungumzia moja ya topic hizi hapa na kuwa mbunifu kidogo au kuzingatia uhalisi wa blog yake basi hatapata taabu ya kupata wasomaji wakudumu wa blog yake.
Mada hizo ni kama :-
1. Blog zinazozungumzia mambo ya sheria (Sheria za Tanzania)
2. Blog zinazozungumzia mambo ya uzazi (Parenting ya kiafrica au kitanzania)
3. Blog zinazozungumzia mambo ya afya za watoto na watu wazima (Dalili na kinga za magonjwa mbalimbali)
4. Blog zinazozungumzia mapishi (ya asilia)
5. Blog zinazozungumzia harusi/ndoa (jinsi ya kufanya matayarisho mbalimbali ya harusi/ndoa, ideas za kufanya sherehe za harusi au mbalimbali, idea za jinsi ya kupunguza gharama mbali mbali za harusi, list ya sehemu nzuri mbalimbali za kufanyia harusi tanzania etc)
6. Blog zinazozungumzia wanyama wa porini na nyumbani.
7. Blog zinazozungumzia bishara, jinsi ya kuanzisha biashara au kuwekeza katika biashara mbalimbali. (entrepreneur blogs)
8. Blog zinazozungumzia Lishe bora (Nutrition) & Fitness
9. Blog zinazozungumzia michezo mmoja moja kwa undani (tennis tu, wrestling tu, badminton tu, soccer tu, swimming tu, netball tu, basketball tu, riadha tu peke yake etc etc)
10. Blog zinazozungumzia au kufundisha hobby mbalimbali kama ( Useremala, kusuka nywele, mashairi, crocheting, knitting, book club, creative writing, michezo ya kuigiza, mapishi, etc)
11. Blog zinazozungumzia safari (traveling) {mfano blog za kuzungumzia sehemu unayoishi kwa undani na vivutio vilivyopo, au sehemu nzuri kwa watu kutembelea kama honeymooners, familia, wafanyakazi au magroup mbalimbali na mambo mengi yanayohusu Tanzania}
12. Blog za wanawake (apart from love, relationship, beauty, fashion and entertainments) {blog zinazozungumzia afya za wanawake kwa ujumla, kuwawezesha wanawake etc}
13. Blog zinazozungumzia uchumi ( uchumi wa Tanzania)
14. Blog zinazozungumzia jinsi ya kutunza hela (financing), jinsi ya kusave a deals mbalimbali zinazopatikana nchini na pia stock market.
15. Blog zinazozungumzia masoko Tanzania (branding, promoting local businesses, etc)
18. Blog za science na technology.
19. Blogs zinazozungumzia real estate na architecture.
16. Blog zinazotumia video (video blogging)
17. Podcast
Najua kuna mada nyingi tu lakini hizi natumaini kuna watu wengi tu wanavipaji au ujuzi wa mambo fulani hapo juu na wangependa kuwaelezea watu wengine.
Check list kabla hujaweka hewani blog yako

1. Hakikisha una post kama tano hivi za kuanzia
2. Hakikisha blog yako ni rahisi kusoma na kuona post zako zingine ulizonazo katika blog yako.
3. Hakikisha una RSS katika home page yako.
4. Hakikisha blog yako inaonekana vizuri kwenye browser mbalimbali. Blog inaweza kuonekana vizuri katika brower moja lakini nyingine ikawa haionekani vizuri. Hivyo jaribu kuifungua blog yako kwenye browswer kadhaa ili kuona inaonekana vipi.
5. Jitahidi uwe na social bookmarking kadhaa kwenye blog yako.
6. Andika kidogo kuhusu wewe hata kama unablog kwa jina lingine ni bora kuwaambia wasomaji wako ukweli.
7. Wape watu wasome tena post zako hizo kabla hujaziweka iwe unaandika kwa lugha ya kiswahili au kingereza. Ni rahisi sana kukosea neno au sentence na usiweze kuona mwenyewe. Na kila mara hisia za kwanza ndio zinawafanya watu warudi au wasirudi tena kwenye blog yako. Hivyo jitahidi sana kila kitu kionekane kuwa kimekamilika hata kama utafanya marekebisho, kuengezea vitu vingine au kubadilisha design ya blog yako baadaye hiyo haina tatizo.
Wako wapi?

Umuhimu wa kushawishi vijana waingie katika hii fan ya kublog ni mkubwa sana na mzuri sana? Najua nchini kwetu kutokana na blog ile ya UTAMU watu wengi wamechukulia blog kuwa ni kitu ambacho ni chakudhalilisha watu tu au ni kazi za waandisha wa habari tu lakini ukweli ni kuwa blogs ni kwa kila mtu na kwa vijana zina saidia sana mtu kufahamu mapenzi ya kitu anachotaka kufanya akiwa mtu mzima mapema sana.
Wengi wetu tulivyokua tunashoma shule za msingi na secondary haya mambo yalikua hayapo. Wengi tulikua tunakwenda shule na kufaulu vizuri lakini mpaka tuna miaka 19 hatujui vizuri ni nini hasa tungependelea kufanya katika maisha yetu. Information zilikua sio nyingi na zilizopo zilikua kutoka kwa walimu au magazeti kutoka kwa wenye bahati ya kuwa na wazazi wasomi.
Ulimwengu tunaoishi sasa hivi ni rahisi sana kupata na kujifunza mambo mengi kupitia katika mitandano. Na jinsi ya kuingia kwenye mitandao sasa hivi sio vigumu sana ukizingatia watu wengi wanatumia simu kuingia kwenye mitandao. Niliona tweet moja kutoka kwa Mr. Chahali inasema “Upatikanaji wa mtandao katika vilongalonga watishia uhai wa maduka ya huduma za mtandao (internet cafes) nchini”. Hivyo vijana wengi sasa hivi wenye kupennda kuwa na blog haitakua vigumu sana.
Mwezi wanne rafiki yangu mwenye mtoto wa miaka 6 aliniambia anamsaidia mtoto wake kutengeza kitabu ambacho mtoto huyo anakiandika. Nilishangaa mtoto mdogo hivyo anaandika kitabu? Rafiki yangu huyo akaniambia ni assignment wamepewa shuleni wakati wa spring break kuwa wakirudi shuleni waandike kitabu cha jinsi walivyospend spring break zao. Nilivutiwa sana na kitendo hicho kwa vile hiyo itawasaidia watoto kujua kumbe hivi vitabu wanavyovisoma kila siku vinaandikwa na watu kama wao. Hata mtu yeyote akitaka kuandika kitabu siku moja basi ni kukaa chini na kuweka mawazo yake pamoja na kuandika. Ukianza kufanya kitu mara kwa mara inaongeza uzoefu na kujiamini hata siku moja ukafanya mambo makubwa kuliko hayo unayozoea kufanya kila siku.
Ni vizuri tukiwahamasisha wadogo zetu, watoto wetu, nieces na nephews kutumia muda wao wanaoingia online vizuri. Blog zinasaidia sana kwa vijana wadogo kujua shauku zao ziliko mapema sana. Blogs pamoja na kuwa zinapeleka habari haraka sana akini sio kila blog lazima iwe ya habari. Unaweza kuanzisha blog ya science, technology, sanaa, utamaduni, Kiswahili, vichekesho, michezo, maarifa ya nyumbani n.k.
Pamoja na kuwa utakua unazungumzia mambo unayoyapenda lakini unajifunza mambo mengi sana pia unapokua na blog kama kuwa na mawasiliano mazuri kati yako na wasomaji wako (communication skills), kuongezea ujuzi wako wa kuandika (writing skills), inakusaidia kuongeza uwezo wako wa kuhariri (editing skills), inakuengezea ujuzi kwenye technology, inakufundisha kufanya utafiti (hii itakusaidia sana ukiwa katika elimu ya juu) au hata kama utaamua kuishia elimu katika level yeyote, itakuengezea ujuzi wa kujua jinsi ya kupublish, kuorganize mambo yako au kuorganize groups, fund raising na mambo mengi tu. Na vitu viwili vikubwa zaidi itakayokuengezea ni kujiamini katika mambo yako mengi unayofanya na kuwa na marafiki mbalimbali au hata nchi mbalimbali wanaopenda mambo unayoyafanya.
Juzi kwenye CNN walikua wanamhoji mtoto ana miaka 11 amezanzisha empire ya mapishi. Pia food channel imeshamtaka huyo mtoto ili wamtengenezee show yake ya mapishi. Huyo mtoto anasema alikua anapenda kupika toka akivyokua mdogo sana na alianza kurekodi picha za jinsi anavyotayarisha mapishi yake na kuweka kwenye youtube. Kutoka huko kwenye youtube ndio biashara yake ya mapishi ikaanza. Kama mtu unakipaji na unakaa nacho ndani nani atakuona au utajuaje kuwa unakipaji kama hutafanya mazoezi au kuwaonyesha watu unachojua? Siku hizi kwa technologia iliyopo sio lazima usubiri kwenda kwenye audition. Mambo mengi ni wewe utakavyojitahidi kujionyesha kwa watu na ulimwengu mambo unayoyajua.
Pamoja na kutembelea blogs za watu kusoma mbalimbali na kuacha comments kila siku (sio vibaya kufanya hivyo) lakini hata wewe unaweza kuwa na blog na watu wakaja kuizoma. Unaweza kuwa na blog pia kama watoto wengine wa nchi zilizoendelea. Sio kufollow blog zao tu kila siku hata wewe unaweza kuwa na blog yako na wao wakafolllow blog yako. Ungejua kuwa kuna watu wengi wanataka sana kujua mambo unayojafahamu pia kama wewe uanvyotaka kufanhamu mambo ya watu wengine.
Mimi (mwandishi wa blog hii) nipo kwa yeyote yule kama kuna kijana yeyote (12-18) yrs old anahitaji msaada wa kuanzisha blog au idesas email ipo hapa....Niandikie mimi natakusaidia kadri nitakavyoweza kuhakikisha una blog yako ya maana. Na pia nitakusaidia kuitangaza.
Umuhimu wa kuweka Meta Tags katika kila blogger post
Jinsi ya kufanya
1. Nenda kwenye Dashboad ya blog yako.
2. Ingia kwenye Design.
3. Nenda kwenye Edit HTML
4. Back up template yako kabla hujafanya chohote...Unaweza kukopy na kupaste kwenye note pad au kudownload kwenye hard drive yako.
5. Tafuta haya maneno kwenye template yako. Kwa urahisi tumia Ctrl+F kuyatafuta....
< title>< data: blog. pageName/> | |
6. Copy haya maneno hapa chini na uweke china ya hiyo line hapo juu.
< meta expr:content='data:blog.pageName' name='description'/ > |
Basi save na umemaliza.
Sasa hii ina maana mtu yeyote atakayekua anasearch kwenye blog yako kwenye google au search engine yeyote ataona jina la blog yako na maelekezo ya kitu anachotafuta kwenye description kutoka katika post yeyote ile. Na utawapita wale wanaoonyesha neno moja moja tu. Sasa maelezo yako kama ni hayo anayotafuta atavutiwa kuingia na kusoma zaidi kwa vile mtari mzimautakua umeonekana hapo.
Ingawaje ukishaweka itachukua kama masaa kadhaa kabla ya kufanya kazi.
Hizi tag kama utaweka vizuri zitaafanya kazi kwney blogger ila nadhani zinaweza kufanya kwenye platform yeyote ile kwa vile zina generate search kutoka kwenye title.
Free Wi-Fi Map Launched
We found this map and thought that it was cool to create for our urban areas too..
The site is designed and built on the Crowdmap platform by the Ushahidi Team from Kenya. Its allows you to:-
- Collect information from cell phones, news and the web.
- Aggregate that information into a single platform.
- Visualize it on a map and time-line.

Arusha Wi-Fi Hotspot Map
We will provide data on all Wi-Fi hotspots located in the heart of these towns/cities. The various categories include:-
- FREE Wi-Fi Hotspots
- Hotels & Guest Houses with Wi-Fi
- Cyber Cafes & Coffee Shops with Wi-Fi
- Winning & Dining Areas
We entrust all dwellers, visitors, bloggers and techies in Tanzania to feed in enough data unto the sites. Visit these sites: Arusha Wi-Fi Hotspots Map, Dar Wi-Fi Hotspots Map, Moshi Wi-Fi Hotspots Map and Mwanza Wi-Fi Hotspots Map and submit reports of all Wi-Fi hotspots you’ve accessed recently. If there are other towns/cities that have these hotspots let us know we will add a map for those cities......
Njia mbalimbali za kutangaza blog yako

2. Peleka blog yako mahali popote penye Blog Directory List au kama kuna mahali pa kuisajili basi iandike. Usisiste kufanya hivyo...kila unapoona mahali kuna list za blog peleka maombi yako na usisubiri wao ndio wakutafute.
3. Omba watu wenye blogs mbalimbali wakutangazie blog yako na kama unafuatilia blog zao ukiona hawajaiweka usikate tamaa kuwaandikia tena. Na ufanye hivi kwa utulivu sio kuwalalamikia watu au kuwalazimisha watu. Kumbuka wewe ndio unahitaji msaada na sio wao na pia ujue kuna bloggers wana ratiba za mambo ya kupost katika blogs zao. Wengine ni ijumaa tu ndio wanapost maaombi ya kila mtu na wengine hata mara moja kwa mwezi tu. Sasa kama hujui ratiba ya hiyo blog au huifuatilii ukituma maombi yako tulia na usubiri hata kwa week kama mbili ndio hapo ujaribu tena kupeleka maombi yako. Ukiwa uanalazimisha kila siku au ukituma maombi yako leo halafu kesho unategemea yawe yamewekwa na usipoona unatuma tena email , utawaudhi watu na mwishowe hawatakuwekea blog yako kabisa. Hivyo uwe na subira....
4. Pitia blog mbalimbali zenye mambo yanayofanana na blog yako na uache comments kwenye blog zao. Lakini uache comments za maana au zinazosaidia na zinazohusiana na topic zilizo kwenye blog yako. H ivyo watu wanaosoma hiyo blog kwa vile interest zao ni sawa na za wasomaji wa blog yako basi wachache wanaweza kuja kusoma blog yako na kama wakikuta mambo mengi wanayapenda basi umejipatia wasomaji wapya.
5. Kama kuna blog umeona mahali inatopic zinazoendana na blog yako na unaweza kuweka link ya blog yako basi fanya hivyo. Ila tricky hapa ni kuwa badala ya kuweka link ya blog yako weka link ya post unayoona inafanana na hiyo blog unayosoma au link ya topic unayoona ni nzuri au ina hits nyingi katika blog yako. Usiweke url ya blog yako yote kila mahali...ukiweka post tu mtu akisoma akavutiwa basi anaweza kupendelea kusoma zaidi blog yako lakini ukiweka Url ya blog na mtu akiingia anaweza akutane siku hiyo kwenye blog yako na vitu ambavyo sio anavyovipenda basi haitakua rahisi kwa yeye kuendelea kusoma blog yako au hata kuikumbuka tena.
6. Mwisho na muhimu ni kujitahidi kila siku kuandika post zako ambazo zina manufaa kwa wasomaji wako. Najua hii haihitaji a rocket scientist kuvumbua lakini ukweli ni kuwa kama post zako sio za muhimu kwa watu wengine hautakua popular na watu hawatajali kukumbuka blog yako. Utakua unapata watu wa kupita tu kila siku lakini watu wakuikumbuka kwa kichwa blog yako, kuibookmark au kumbuka kufungua blog yako kila mara wanapopata muda hautapata kabisa. Kama unacopy habari za watu wengine ambazo wameshazitangaza kwenye blog zao nani anajali? Kama wewe ni wakuelezea jinsi siku yako ilivyokua chuoni kwako, kazini kwako au jinsi ulovyospend weekend yako nani anajali? (Labda kama wewe ni mwandishi mzuri ) na ukielezea unaandika kwa lugha ya kuvutia watu bila hivyo utakua unapoeteza nguvu tu hata huko unakojitangaza itakua nihasara tu. . Jitahidi kuandika mambo ambayo ni muhimu lakini sana sana jitahidi kuandika mambo yako yawe unique na organic na watu wote watakukimbilia kila siku mara wakishaifahamu blog yako kutaka kujua kesho kutakua na nini??????
Umuhimu Wa Kuitangaza Blog Yako Kila Siku Upatapo Nafasi

Watu wengi wanafikiria kuwa kwa sababu wana blog na labda ina mambo mengi basi inajulikana sana. Ukiwa na blog up and running haimaanishi kuwa utapata wasomaji wa kusoma blog yako mara moja au kwa vile blog yako inapata 1000 hits kwa siku haimaanishi kuwa blog yako inajualikana na kila mtu. Watu wengi wananitumia email na kulalamika kwanini sijaiweka blog hii au ile kwenye Directory List yetu. Wengine wanafikia hata kusema blog zao ni mashuhuri sana kwa nini sijaziweka kwenye Directory List yetu mpaka sasa hivi. Sasa cha muhimu ni kuwaambia watu wote wanaoblog, hata siku moja usiache kuitangaza blog yako kwa vile unaona una hits 1000 au zaidi kwa siku. Kwanza hizo hits hazimaanishi kuwa ni number ya watu waliotembelea blog yako hiyo siku. Hiyo inamaanisha number za pages zilizofunguliwa katika blog yako kwa siku hiyo. Hivyo kama mtu mmoja ameangalia post mbalimbali ndani ya blog yako na pia kama amehit the refresh button hata kama ni kwenye ukurasa huo huo basi hit counter itakua inaongezeka tu. Anaweza kuondoka na kusoma vitu vingine na baadaye kurudi tena kwenye blog yako hit counter itaongezeka. Na mtu huyo huyo anaweza kurudi kusoma blog yako kila siku na hata mara zaidi ya moja kwa siku. Hivyo hizo 1000 counts zinaweza zimetokana na watu 100 tu au pungufu. Hivyo unatakiwa ujue hili hata siku moja hit counts 1000 sio kuwa watu 1000 wamesoma blog yako kwa siku hiyo.
Na pia watu wengine wanafikiria kuwa kwa vile blog zao zinajulikana sana na watu fulani au na kundi fulani basi wanafikiria kuwa kila mtu anaijua. Blog yako inaweza ikawa maarufu mahali fulani lakini bado kuna watu hawaijui mahali pengine. Inaweza ikajulikana sana nchi fulani lakini haijulikani nchi nyingine. Hivyo usiache kuitangaza blog yako kila unapopata nafasi. Tukichukua mfano wa makampuni makubwa na mashuhuri kama Pepsi au Nike ambayo wengi wetu tumezaliwa na kuzikuta hizi brands. Ingawaje zinajulikana sana lakini kila mwaka wanatenga fungu la kutumia katika matangazo ya bidhaa zao. Sasa kwa watu ambao hawajasomea biashara itabidi ujifunze kitu kimoja hapa. Kampuni kama hiyo ambayo wewe unafikiria kila mtu anaijua kwanini inatumia hela zake nyingi tena katika matangazo? Si wangeacha tu kwa vile watu wengi wanazijua? No!!!! Katika ulimwengu wa biashara na mfanya biashara wa kweli hata siku moja hatakiwi kufikiria kuwa kwa vile kitu chake anachouza ni maarufu basi hana shida ya kutangaza tena.....Lazima kuna mtu mmoja atakua hajui na hata kama akiwa anajua basi kuna ushindani wa bidhaa nyingine hivyo unatakiwa uwakumbushe wateja wako umuhimu wa biashara yao au kama umebadilisha vitu kadhaa katika biashara yako. Msomaji wa blog yako ni kama mteja wako unatakiwa umkumbushe mara kwa mara na uweshimu. Ingawaje labda blog yako ni kwa ajili ya kufundisha au kutangaza lakini bado ujue kuwa hao watu unaotaka kuwafundisha ni vizuri kuwaheshimu hata kama unajua kuwa unachokiandika kinawanufaisha.
Hivyo ili usikate tamaa ya kublog, mwanablog yeyote anayetaka kufanikiwa anatakiwa juhudi zake za kutafuta vitu vya kuweka katika blog yake viende sambamba na juhudi za kutafuta jinsi ya kutangaza blog yake kila siku. Bila hivyo utaishia kuwa unablog tu peke yako tu kila siku. Kila unapojitangaza hata ukiongeza mtu mmoja kuifahamu blog yako ni heri kuliko ungekaa tu kimya.
Baada ya hayo ninalotaka kukwambia ni GOOD LUCK kublog sio kazi rahisi lakini ni very rewarding thing to do. Na kila siku ukumbuke kublog iwe funny au topic unazo blog uwe unazipenda kama huenjoy au hupendi topic unazoziblog humo hutafika mbali bora uache.
Jinsi ya kuanzisha blog
Nimejaribu kuandika kwa Kiswahili kama watu walivyoniomba sasa kama kuna kitu nitakosea au nimeacha basi naomba usiache kuniandikie ili nisahihishe.
Kuwa na blog ni bure na hamna kitu ambacho unatakiwa kulipia zaidi ya muda wako utakao tumia kwenye internet. Kama unataka kuwa na jina lako binafsi mfano www.Tanzania.com na kuhost wewe mwenyewe basi hapo ndio utatakiwa ulipie lakini kama blog yako itakua kama http://tanzania.blogspot.com basi hutalipia chochote. Na kama wewe ndio unaanza tu kublog na hujajua unataka kublog nini basi ni vizuri kutumia blog host za bure mpaka hapo utakapoelewa zaidi na kama ni kutaka kuipeleka blog yako mbali zaidi basi utajua mwenyewe hapo baadaye. Na faida ya hizi blog za bure ni kuwa unaweza kubadilisha jina la blog yako wakati wowote kama hilo jina unalotaka kulitumia bado halijatumiwa na mtu mwingine.
Blog zinaweza kuwa katika platform kadhaa kama:-
Blogger - www.blogger.com
Wordpress - www.wordpress.com
Typepad - www.typepad.com
Posterous - www.Posterous.com
Letterdash - www.letterdash.com
Tumblr - www.tumblr.com
Sasa mimi hapa nitaandika maelekezo ya jinsi ya kuanzisha blog kwa kutumia platform ya blogger.com ambayo naiona ndio rahisi sana kwa mtu yeyote kutumia na ambaye hana ujuzi mwingi lakini hii ni kwa mawazo yangu tu. Unaweza ukaenda kuangalia hizo zingine zinaweza zikawa kwako ni rahisi kuliko hii hapa.
Nenda hapa www.blogger.com
Utaona mahali panasema “Create Your Blog Now"Kama huna google account basi jaza maelekezo hayo hapo juu. (Gmail account)
Kama una account basi pita haya maelekezo na kutumia “sign in with existing account”
Ipe jina blog yako..Kama hutumii jina lako basi jitahidi jina hilo liwe fupi na liwe linaendana na vitu utakavyoweka kwenye blog yako.
Tafuta design unayotaka iwe katika blog yako.
Umemaliza sasa na wewe unablog yako
Natumaini haya maelekezo yatawasaidia wale waliokua wanataka kufahamu jinsi ya kuanzisha blog.