Kutana na Mwanablogger Augustino Chengula




Unaweza kutuambia kidogo kuhusu wewe na blog yako?
Mimi naitwa Augustino Chengula niliyehitimu shahada ya kwanza ya Tiba Mifugo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro mwaka 2007. Blog yangu inaitwa “SEKTA YA MIFUGO TANZANIA” inayobeba jina linaloendana na kile kinachowasilishwa katika blogu hiyo. Lengo kubwa la blog ni kuelimisha umma na wafugaji juu ya ufugaji na namna ya kukabiliana na magonjwa ya mifugo.

 Je, wewe kazi yako ni kublog tu au hii ni kama kazi ya muda tu au hobby?
 Kublog si kazi yangu ila ni hobby tu na lengo langu kubwa ni kuelimisha umma na hasa wafugaji juu ya mifugo na ufugaji na mambo yanayoendana na hayo. Hivyo naelimisha umma kwa kupitia fani yangu ya mifugo.

Jinsi gani unaanza kublog na kwa nini?
Kabla hata ya kuanzisha blog nilikuwa najaribu kutengeneza tovuti yangu kwa kupiatia zile za bure. Baadaye nikaona kwa kuchelewa watu wanablog na mwanzo sikujua kama ni za bure. Nilipojua kuwa ni za bure nikaanza kujifunza mwenyewe namna ya kufungua blog, nikafanikiwa. Nikawa naendelea kuiboresha taratibu kwa kuangalia blog za watu wengine zipoje. Wakati mwingine nilitumia Jamii forum kuuliza kama nataka kufanya kitu fulani kwenye blogu inakuwaje. Sikuwa na elimu ya web designing lakini nilijua kutumia vitu vya kawaida katika computer. Kupenda kujifunza vitu mwenyewe vilinisaidia. Lengo kubwa la kuanzisha ni kutaka kuwagawia elimu ya ufugaji watu wengiene kwani niliona wanahangaika kuitafuta hasa katika lugha ya kiswahili kwani mambo mengi yapo kwa lugha ya Kiingereza.


Nini changamoto unazozipata kwa kuwa na blog?
Changamoto ni muda kwani watu wengi wanahitaji elimu hii ya ufugaji na wengine wanahitaji kujua vitu vingi sana. Kwa kuwa ni kazi nyingine mara kadhaa nakosa muda wa kuweka elimu mpya kwenye blogu kila siku. Nahitaji watu wa kunisaidia hasa kuchukua matukio huko mifugo iliko na kuwajulisha watu wengine. Lakini pia kuandaa mafundisho ya ufugaji yanahitaji muda na utulivu hivyo kushindwa kuweka kwenye blogu kila siku.

             Unafanya nini wakati ukiwa hushughulikii hii blog yako?
Nakuwa na majukumu mengine ya kikazi

Ni mara ngapi unafikiri juu ya blog yako wakati uko mbali na kompyuta?
Mara nyingi sana kwani natamani watu waipate elimu ya ufugaji kwa wingi iwezekanavyo

Ni nani wasomaji wa blog yako?
Ni watu wote wanaofuga, wasiofuga na wanaopenda kuingia katika fani ya ufugaji. Elimu hii inawasaidia pia wasiofuga kwani kuna magonjwa yanayoweza wapata kutoka na kula nyama ya mifugo au mazao yake au wanaweza kuambukizwa hata bila ya kuwa na mifugo.

Je ni mitandao gani mingine ambayo unatumi ili iweze kukusaidia kuitangaza blog yako ili iwafikie wasomaji walengwa wa blog yako? 
Mitandao ninayotumia ni: Facebook (nina facebook page inayoitwa Sekta ya Mifugo Tanzania), twitter, Jamii forum na google na yahoo groups.

Nini hasa ni changamoto kubwa wakati unatengeneza posy ya kuweka kwenye blog yako na kwanini?
Uwekaji wa post kwangu hauna changamoto yeyote


Unafanya nini iwapo kuna wakati huna la kuandika kwenye blog yako?
Siwezi kukosa la kuandika kulinga na sekta ilivyopana na ina mambo mengi ambayo wafuatiaji wanataka kuyajua. Tatizo ni muda tu.

 Je ni nini mkakati wako na blog yako kwa ujumla?
 Mkakati wangu ni kuendelea kuiboresha na kuweka post za kuelimisha mara nyingi iwezzekanavyo. Na nikipata watu wa kunisaidi hasa huko mifugo iliko wenye nia ya kuelimisha watu bila kujali pesa itanisaidia sana kuifanya blog yangu ikue na kupendwa na watu wengi zaidi.

Je ni bora kupata ukweli au uchunguzi wa jambo unalotaka kuliandika kwenye blog yako wewe mwenyewe au kupitia mtu mwingine?
Kupata ukweli ni muhimu sana si lazima utoke kwako mwenyewe bali kwa mtu unayemuamini kuwa ni mkweli.

Ni jambo gani bora blogger anaweza kutoa kwa wasomaji wake?
 Japo bora ni lile lenye msaada kwa msomaji na si uongo, uzushi au jambo lenye kugombanisha. Linapaswa liwe na manufaa kwa musomaji na si hasara.

 Ni jinsi gani (mtu) anaweza kuelezea style ya yako unavyo blog?
 Style yangu ya kublog siku zote ni kutoa elimu kwa umma bure

Ni nini imekuwa mkakati wako kwa ajili ya kujenga kujulikana kwa mwenyewe na blog yako?
Kwa sasa ni kutumia mitandao ya kijamii

Je ni bloggers wapi ambao wewe unawaangalia na kufuata nyayo zao? Na kwanini?
Issa Michuzi hasa namna anavyotafuta habari kwa wingi, anavyoboresha blog yake na ulinzi aliouweka kwenye blog yake. Natamani name niiboreshe blog yangu lakini najua inahitaji pesa ili utumie wataalamu waweze kuiweka katika muonekano unaoutaka. Kwa sasa bado siajfikia pale ninapotaka angalau nifike.

Hebu tuambie ni watu gani umewahi kukutana nao wakati ukisughulikia post za kuweka kwenye blog yako?
Mara nyingi nakutana na wafugaji

Je unafikiria kuwa unadaiwa na mtu akiyeacha comment/s kwenye blog yako?
Sidaiwi

Je kunadhamani kujibu comment iliyoachwa kwenye blog yako wakati ukijua kuwa huyo aliyeiandika labda hatarudi kusoma jibu lake tena?
Thamani ipo, hata kama hatarudi itawasaidia wafuatiliaji wengine na huenda kuna wengine wanaweza kuwa na maswali kama yake.

Je, umewahi kufikiria kuacha kupost comment ambayo iko negative kwako na ukijua hamna mtu atakayejua?
 Zijawahi

Je unazitreat tofauti au unafikiri watu wanaoacha comment kwenye blog yako na kuacha majina yao yaonekane wazi wanastaili comments zao kujibiwa au hata kuacknowledge kuwa umeona maoni yao?
Comment zozote zina maana sana hivyo ni muhimu kuzijibu kulingana na zinavyotaka ujibu. Hazipo kwa bahati mbaya, ila majibu yawe na busara ndani yake. Pia comment iwe ya kimaadili isikiwuke maadili ya Kitanzania

Je, unafikiria ni makosa kucomment kwenye blog yako kwa kutumia jina lingine?
Si makosa, ilimradi tu comment iwe na maadili kama si ya kimaadili au haiendani mambo yaliyo kwenye blog haifai.

Je unazichukulia comments zote sawa unazotumiwa kwenye blog yako bila kujali maoni uliachwa?
Kama zina mlengo wa blogu yangu, zote nazipa uzito sawa

Je, unaamini comments kwenye blog yako zilizoandikwa kwa urefu sana zinahitaji kuzawadiwa zaidi kuliko zile zilizoandikwa kwa ufupi tu?
Hapana hapa swala si ufupi au urefu wa comment bali ni uzito wa ujumbe ulioko kwenye comment

Je wewe ni mtu ambaye uko rahisi kukata tamaa?
Si kati tamaa kirahisi kwani unapokaribia kukata tamaa ndipo mafanikio huanzia. Hivyo naongeza bidii ninapokaribia kukata tamaa

Je unaedit picha zako ili ziwavutie sana wasomaji?
Si kila picha kwani muda kwangu ni tatizo hivyo si zote huwa naziedit

Je unaepuka kuweka post ambazo ziko very controversy kwasababu ya kuogopa watu hawatakubaliana na wewe au huna hizo post?
Sina hizo post

Je  unajisikia vizuri zaidi ukiweka post kwenye blog yako na ukapata maoni ya watu zaidi ya 20 au ukipata maoni ya mtu mmoja mashuhuri tu.
Maoni ya wengi ndiyo ninayo yapenda kwani yananijenga na kunipa mwanga
  
Je unasema blog yako kuwa inamafanikio iwapo unapata watu wengi wa kusoma  au unapata watu wengi wakuacha comment kwenye blog yako? 
Mafanikio ya blog yangu ni pale watu wengi wanapo itembelea na kuisoma, na    wanapoacha comment wengi ni ishara kuwa wengi wameisoma na kupata ujumbe husika.

Je blog yako unatumia jina lako kamili au unablog kwa kutumia kivuli kingine na watu wanasoma na kuenjoy blog yako lakini hawajui wewe ni nani?  
Blogu inatumia jina la kile ninachoelimisha, address ya blog imebeba jina langu na chini ya blog kuna jina langu halisi na kazi yangu ninayofanya. Hivyo wasomaji wa blog wanajua ni blog ya nani.


Ni nini baadhi ya malengo yako ya mwaka huu kwa ajili ya blogu yako au unaonaje mwenyeew kwa kipindi cha mwaka mmoja ua mitano toka sasa hivi blog ya itakuaje? 
Malengo yangu ni kuitangaza zaidi watu wengi waijue kwani naamini wapo wengi wanaopenda kupata elimu hii kwa kiswahili, lakini bado hawajafanikiwa kuijua. Pia ndani ya miaka mitano ijayo naamini nitakuwa na watu huko kwa wafugaji watakao nisaidia kukusanya habari za mifugo na ufugaji ili tuwasambazie watu wengine.

             Je upi ujumbe wako kwa wale watu wanaotaka kuanza kublog?
Lazima waanze na malengo ya kwa nini wanataka kublog, na wasilenge pesa walenge kutoa habari au kuelimisha na wawe na nia hiyo ya dhati. Wakilenga pesa wasipopata wataishia kukata tamaa.

Je kwa maoni yako ni lengo gani kubwa kwa mwanablogger?
 Lengo kubwa ni kutoa habari na kuelimisha

Watu wengi wanafikiria kublog kwa ajili ya kupata hela. Je ni nini baadhi ya vidokezo kwa watu wanaofikiria kufanya hivyo? Je, ni ukweli upi wa baadhi ya matarajio yanayohusina na nini kinaweza kufanywa na nini hakiwezi kufanywa wakati wa kublog?
Akiwa na malengo ya kupata hela inabidi awe amejipanga sana, kwa maana hiyo itakuwa kazi ya kujiajiri na itategemea sana jitihada zako. Vinginevyo utaishia kukata tamaa, huwezi kuanza leo kublog halafu kesho utegemee kupata pesa. Kazi si kuanzisha blog, kazi ni kuitangaza na kuwavutia watu wengi kuitembelea.

No comments: