Mwana blogger wa week hii ni Nixl Carter



Mimi naitwa Nickson Lema lakini ni maarufu kwa jina Nick au Nixl Carter ni mkazi wa Moshi.

Nimekua blogger kwa muda wa mwaka 1 na nusu .Kiukweli Nilivutiwa kuanza blogging baada ya kuwa napata habari mbalimbali na kuona zinafaa kuwafikia watu wengine so nikawa pia na muda wa kufanya blogging, pia ubunifu wangu uliniruhusu kuweza kuanza na kupata idea nzuri. Kwa Kuanza nilianza na blog ya Jokes na Funny stories (SUPAJOKES) www.supajokes.blogspot.com lakini nikawa pia interested na issue za entertainment nikaona ni vyema niwe na blog kuhusu burudani,music,habari na pia chatting, ndipo mwaka wezi wa tisa mwishoni nikaanzisha blog ya (BONGO SWAGGZ) www.bongoswaggz.blogspot.com


 


Kublog sio kazi yangu huwa nafanya kama hobby mimi nasomea mambo ya mambo ya markerting na Business katika chuo kikuu cha Tumaini.

Nakutana na Changamoto nyingi kama kupata vitu/habari ambazo ni unique na za kweli, pia vitendea kazi
kama kamera ni changamoto kwangu. Wasomaji wa blog yangu ni watu wa rika zote kwani blog yangu ina habari zinazomhusu kila mtu.

Style ninayotumia kublog ni ile inayoambatana na picha za matukio husika au hata kama sina picha za matukio husika hua natafuta picha za wahusika kupitia mitandao mingine ili kufanya post ziwe na mvuto zaidi. ingawa kuna baadhi ya habari picha zake zinaitaje editing.

Bloggers ambao wamekua kioo kwangu na ambao natamani nipite katika njia walizopita ni Issa Michuzi, John Kiandika, Josephat Lukaza na Dj Coka. Nawakubali kwani wanafanya kazi nzuri na makini kila mara.

Ni vizuri kufanya uchunguzi wa jambo kabla ya kuliandika kwenye blog.

Mtuakiacha comment lazima nimjibu lakini kutegemea na alichoandika kama ni swali nitamjibu au anaitaji kufahamu chochote atajibiwa

Kukata tamaa katika maisha ni kitu ambacho nawezakusema kuwa nidhambi kwani kila mtu anayo akili na uwezo wa kufanya kazi na matunda yake yakaonekana pia yakawa na faida.
Malengo yangu kwa mwaka huu ni kupata wasomaji wengi katika blogs zangu sana katika blog hii mpya ya Bongo Swaggz pia kufikia watu katika kila kona ya dunia.

Ujumbe wangu ni kwa wanaotaka kuanza kazi hii ni kuwa wasikate tamaa mwanzoni kwani mwanzo huwa mgumu lakin juhudi huleta njia.

Nadhani lengo la Bloggers ni kuwa na wasomaji wa kudumu na kuweza kujitengenezea kazi yenye kipato.


Thanks Nixl ..Tunakutakia mafanikio mema katika masomo yako na blog yako pia

No comments: