Bloggers Association & Shindano la Mwaka huu

Okay guys ...Naona watu wengi hawakuitikia wito wa Bloggers Association of Tanzania, hivyo hiyo site nimeiondoa na jina linaexpire mwezi ujao hivyo sita renew tena.....Nilikua natafuta mahali pa kusalvage shindano hii ambalo linaonyesha bado kupendwa na watu wengi.

Baada ya kusema  kuwamwaka huu sitaweza kufanya shindano hili peke yangu bahati nzuri kuna uwezekano wa shindano hili kudhaminiwa na kampuni moja ua makampuni kadhaa yaliyopo Tanzania...Sio kuwa ni kundi la watu wanalichukua kama hapo nilivyotangaza bali ni kampuni kadha za Tanzania (majina tutayatangaza) kila kitu kikisha kamilika watadhamini shindano hili. kwa mwaka mmoja au kila kila mwaka  pia hilo bado sijajua. Habari kamili na kampuni hiyo au hizo tutawaeleza kila kitu kitakapo kamilika. 

Hivyo tusije kulaumiana vitu vikiwa tayari itatangazwa na hiyo kamati ikiamua ni tarehe ngapi itatangazwa. Make sure everything is ready to go with your blog...Ikiwa na maana hakikisha una update blog yako often na ina quality inayohitajika.

Muda wa shindano utatangazwa. Zawadi zitatangazwa na siku ya kukabidhi zawadi hizo zitatangazwa... Mahali pa sherehe za kupokea zawadi hizo 100% itakua ni Dar Es Salaam, Tanzania. 

Kutakua na kundi linalosimamia hivyo uteuzi wao ndio utakua wa mwisho... Hivyo anza kuhakikisha wasomaji wako wanafollow up na blog yako na wapo aware na wawaambie wenzao. 

Good luck.......

No comments: